Sunday, April 27, 2014

FUVU LA KICHWA CHA BINADAMU NA MIKONO YAMEONEKANA APRIL 26 KWENYE MTO WAMI WILAYANI KILOSA



Mabaki ya mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari kilosa aliyefahamika kwa jina la Protas masinde yameonekana April 26 katika mto wami rudewa
.
Akizungumzia tukio hilo mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amesema kuwa mtoto huyo amepotea tangu April10 ya mwaka 2014 na juhudi za kumtafuta hazikuzaa matunda.
Aidha Tarimo ametoa wito kwa wanafunzi kufuata maelekezo pindi wawapo shuleni kwa kueleza kuwa marehemu na weenzake wawili walitumwa kuchota maji iliyo salama lakini wao walienda sehemu nyingine na kusababisha madhara hayo.Pia ameongeza kwa kusema kuwa kutokana na miundombinu ya maji kuharibiwa na mto shuleni hapo na kuwalazimu wanafunzi kwenda kuchota maji mtoni kwa ajili ya shughuli mbalimbali pia Halmashauri ya wilaya ya kilosa imejipanga kukarabati miundombinu hiyo ili kuepusha usumbufu na upatikanaji wa maji shuleni hapo.

Pia Baba mkubwa wa mototo Raimond Tangaraza amesema wamesikitishwa sana na taarifa hiyo lakini amesema kuwa kazi ya mungu haina makosa na licha majonzi hayo anawashukuru viongozi,wananchi na majirani kwa msaada wao waliouonyesha katika utafutaji wa mwili huo wa mototo wao.

Aidha mwalimu mkuu wa shule hiyo Erasto Lulandara amesema kuwa mwanafunzi huyo amepatwa na umauti huo alipoenda kuchota maji akiwa na wenzake sehemu ambayo maji yanachemka na amesema kuwa ni sehemu yenye kina kirefu ndipo Protas alipotumbukiza ndooyake kwa ajili ya kuchota maji ndipo ndoo ikamtereza na na alipojaribu kuidaka ndipo alopotereza na kuzama majini.

Kwa upande wake shuhuda wa tukio hilo Saidi Ally amesema kuwa wamekuta mwili wa marehemu ukiwa ni vipandevipande abavyo ni fuvu la kichwa,mikono na sehemu ya mwili na kusema kuwa chanzo cha kugunduliwa kwa mwili huo watoto waliokuwa wanavua samaki katika mto huo ndipo walipounasa mkono wa marehemu na kuongeza kuwa wameukuta mwili huo ukiwa katika hali mbaya.

Naye mganga mkuu wa hospitari ya wilaya ya kilosa John Nkinda amethibitisha kuwa ameupokea mwili huo ukiwa katika hali ya vipandevipande majira ya saa 8 mchana ya April 26 na kueleza kuwa wameuhifadhi chumba cha kuifadhia maiti na wanawasubiri  ndugu wa motto huyo kuja kuchukua mabaki ya mwiliwa marehemukwa ajili ya shughuli za mazishi.

Aidha kamanda wa polisi mkoa wa morogoro Paulo Leornad amesema kuwa amepokea taarifa hizo april 27 na kuahidi kutolea maelezo April 28 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment