Tuesday, April 15, 2014

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 14 AFA MAJI WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO.



Zoezi la kumtafuta mwanafunzi wa shule ya sekondari Kilosa  alietumbukia kwenye maji na kupotea katika mto wami bado linaendelea katika kijiji cha Ludewa  gongoni Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.

Akizungumza na HABARIKWANZA  mwalimu Mkuu wa shule hiyo Erasto Lulandala amesema kuwa mwanafunzi aliyetambulika kwa  jina la Protasi Masinde Stansilaus mwenye umri wa miaka 14 alitumbukia mtoni sehemu yenye kina kirefu mwishoni mwa wiki iliyopita. Akizungumzia tukio hilo mwalimu huyo aliongozana na wanafunzi wenzake wawili waliojulikana kwa majina Julias Mathias na Kapungu Kiwangu wanaokadiliwa kuwa na umri wa miaka 14 ambapo walienda  mtoni kuchota maji ya kuoga na ndipo mtoto huyo alipotumbukia kwenye maji na kupotea.

Kwa upande wake Baba Mkubwa wa mwanafunzi huyo Raimond Tungaraza  amesema kuwa matumaini ya kumpata mtoto ni mdogo kwani tangu apotee ni  siku ya tano na hali ya hewa inazidi kuwa mbaya kwani mvua zinanyesha na maji yanaongezeka kila siku. Tungaraza amesema kwa sasa wanaendelea kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Rudewa gongoni kikosi cha uokoaji pamoja na askali polisi kumtafuta mwanafunzi huyo.

Naye kamanda wa polisi mkoani Morogoro Faustine Shilogile amesema kuwa tukio hilo la mtoto kupotea kwenye maji kuwa hawezi kutoa majibu kama amefariki au laa na majibu zaidi yatapatikana hadi pale atakapopatikana.

No comments:

Post a Comment