Tuesday, April 1, 2014

WAKAZI WA MAGOMENI WILAYANI KILOSA WAENDELEA KUTESWA NA MAFURIKO



Mwnyekiti wa kitongoji cha Mbwamaji  kata ya Magomeni Wilayani Kilosa Emmanuel Mwendapole amewataka wakazi wa magomeni waishio mabondeni  kuhama mapema kuepukana na mafuriko yatakayo waathili katika makazi yao.

Kwa mujibu wa Mwendapole amesema kuwa kitongoji chake kilivamiwa na maji mnamo march 29 na kuwaadhili wakazi  56 waishio katika kitongoji chake, Pia  Mwendapole  ameiomba serikali kuwajengea tuta litakalo zuia maji , maji yatokayo mtoni na kuvamia  makazi ya watu pia ameongeza kwa kusema kuwa anawataka wananchi kuacha kulima pembezoni mwa mto huo wa mkondoa ili kujihami na mafuriko hayo.

Aidha wahanga hao wa mafuriko hayo Mohamedi Mungumbele na Lussia Joseph  wamesema kuwa mafuriko hayo yameathili kuanzia mazao ya mashambani vyakula pamoja na mifugo. Na kusema kuwa baadhi  ya vitu  vimeharibika ikiwemo vitanda na vyombo

No comments:

Post a Comment