Friday, April 11, 2014

WANAKIJIJI WA KATA YA MBUMI WATAKIWA KUWA NA SUBIRA JUU YA MAREKEBISHO YA MFEREJI .



Wakazi wa kata ya mbumi A wilaya ya Kilosa mkoani morogoro wameilalamikia serikali kwa kutowafanyia marekebisho mifereji ya kupitishia maji na makaravati kwa kutokuwa na ubora.

Hayo yameelezwa April 10 mwaka huu wanakijiji wa Mbumi “A” kata ya Mbumi wilayani Kilosa , waliovamiwa na maji yaliyopasua kutoka mifereji na kusababisha madhara katika makazi yao.
Aidha baadhi ya wanakijiji hao waliothilika na maji hayo Ally Nassoro Mkelewe na Magreth Msonge wamesema kuwa wametoa malalamiko yao kwa muda mrefu lakini serikali bado haijawatekelezea mahitaji  yao kwa kusema kuwa makaravati yaliyopo yapo chini ya kiwango kwani yaliyopo ni makaravati yenye urefu wa CM 60 na  machache ni ya cm 90 . Na kuongeza kuwa makaravati yanayohitajika ni yale yenye urefu mzuri wa kupitisha  maji kiurahisi. 

Aidha mwenyekiti wa kitongoji cha Mbumi “A” Ally .S. Ngata amesema kuwa wakazi wake wameathiliwa na maji hayo na kueleza kuwa zinahitajika jitihada za karaka kuweza kuokoa mali za watu pamoja na miundombinu na kuongeza kuwa anawaomba waandisi kutembelea eneo la kwa Ngola kuona jinsi maji yanavyopita kwa urahisi kutokana na mfereji kuwa mrefu na karavati zenye ubora zenye uwezo wa kupitisha maji mengi kwa haraka.

Naye mwenyekiti wa mji mdogo Kilosa Ally .S. Malingo amesema kuwa maji yanayowasumbua wakazi wa mbumi “A”  ni yale yale yanayotoka manzese ambapo kulikuwa na miti mingi na ilikuwa inapunguza maparomoko ya maji ambapo kwa sasa kuna makazi ya watu na kusababisha maji kuporomoka kwa kasi na karavati zilizopo kushindwa kuhimili maji . Aidha Malingo amesema kuwa ifikapo june mwaka huu serikali itaanza ukarabati wa maeneo yaliyoharibika na kuwataka wanakijiji kuwa na uvumilivu kwa kipindi hiki.

No comments:

Post a Comment