Friday, July 11, 2014

DAKTARI FEKI AKAMATWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA MOROGORO




Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Renard Paul
Polisi mkoani morogoro inamshikilia Karume Kauzu Habibu Mkazi wa Riti kwa kujifanya daktari katika haspitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro ambapo  amekuwa akioneka maeneo hayo huku akiwa mevalia mavazi ya udaktari. 

Kamanda wa polisi mkoa wa morogoro Kamishana Msaidizi Mwandamizi wa jeshi la Polisi Renard Paulo amethibitishwa kutokea kwa tukio hilo na amesema mtuhumiwa  huyo baada ya kukaguliwa amekutwa na vitambulisho vinne tofauti huku kingine kikionyesha anajiandaa kurudia mtihani wa kidato cha nne, makazi yake yakiti RITI mkoani Morogoro na huku kitambulisho chake kimoja kinaonyesha kuwa alikuwa anasoma Kigoma. 
Daktari feki aliyevaa koti jeupe Karume Kauzu Habibu akiwa chini ya ulinzi
Baadhi ya Vitambulisho vya daktari huyo feki.































  Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji Francis Semwene amesema alipata taarifa toka kwa muuguzi wa zamu na kuweka mtego ulifanikisha kukamatwa kwa daktari huyo feki.

Matukio kama haya yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara nchini kwa baadhi ya watu wasio waaminifu kujiingizia vipato kwa njia zisizo halali na kutishia usalama na afya za wananchi.

Waandishi wa Habari nao Hawakuwa nyuma

No comments:

Post a Comment