Monday, July 7, 2014

UKATILI WA KIJINSIA SASA BASII



Shirika la usaidizi wa kisheria mkoano morogoro Paralegal limeendesha mdahalo wa kupinga ukatili wa kijinsia julai 5 mwaka huu wilayani kilosa mkoani mkoani morogoro.
Akizungumza katika mdahalo huo Meneja wa shirika hilo mkoani morogoro Flora Masoy amesema kuwa wanatoa mafunzo hayo  kwa wananchi ili waweze kujitambua na kutokomeza  vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia ambavyo mara nyingi vitendo vya ukatili hufanyiwa akina mama pamoja na watoto.

Ameongeza kwa kusema kuwa kinamama wengi hutendewa ukatili wa kijinsia na kubaki kimya kutokana na hofu wanayopewa na wanaume zao na kuwataka kina mama kuacha kukaa kimya kwani nao wanahaki sawa na mwanaume na kukaa kimya kwa mwanamke ni sawa na kujikatili wewe mwenyewe na kuwaomba kina mama na jamii kiujumla kufichua maovu yote ya unyanyasaji wa kijinsia bila kuwa na hofu yoyote.
                                                   Wajumbe wakiwa kwenye mdahalo

Wakizungumza katika mdahalo huo baadhi ya wajumbe katika mdahalo huo Baby Mussa na Stella Venus wamesema kuwa wanalishukuru shirika la Paraleg kwa kutambua maovu yaliyoko kwenye jamii  na kuamua kuhamasisha wananchi kuachana na ukatili wa kijinsia kwa kutumia midahalo hiyo na kuongeza kuwa wanaomba katika mchakato wa kuipata katiba mpya wajumbe waliangalie swala la usawa kati ya mwanamke na mwanaume katika jamii .

Aidha wamesema kuwa waliyoyapata katika mdahalo huo kwenda kuyatendea kazi katika jamii zao wanapotoka na kuhahakikisha kila mtu anapata haki yake kwa kusema kuwa kwa wilaya ya kilosa wanaume wanaume hutelekeza familia kwa mwanamke, mwanamke kuamrishwa kutozaa na mwanamke kukosa haki yake ya kimsingi katika ugawaji wa mirathi na kusema kuwa watasimama imara katika kupatikana kwa haki kwa kila mtu.

                       Mmoja wa wajumbe wakiwa kwenye mdahalo wakijadiliana kuhusu ukatili wa kijinsia


        Wajumbe wakiwa kwenye vikundi kujadiliana kuhusiana na mada ya ukatili wa kijinsia

No comments:

Post a Comment