Thursday, July 3, 2014

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA MITATU ATELEKEZWA NA MAMA YAKE MZAZI WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO


Mama mmoja anayefahamika kwa jina la Mwamini Juma [20] mkazi wa mamoyo wilayani Kilosa mkoani Morogoro anadaiwa kumtelekeza motto Selemani Salumu mwenye umri wa miaka mitatu (3) kwa shangazi zake naye kwenda kwa wanaume.

Kwa majibu wa shangazi zake Mwamini Juma ambaye  ni mwasham Salumu na Halka Salum wamesema kuwa motto wao huyo mwamini salumu ambaye ni motto wa kaka yao anatabia ya kumtekeleza mtoto mara kwa mara na kwenda kwa wanaume wengine huishi nao na mwisho wa siku naye huachwa.

Aidha wamesema kuwa mtoto Mwamini Juma alipewa mimba akiwa na umri wa miaka 17 na kijana anayefahamika kwa jina la Doto salumu mkazi wa mamoyo wilayani Kilosa mkoani Morogoro ambapo mwaka 2011 alimpa mimba mtoto waliongea juu ya matunzo ya mtoto na kukubaliana katika malezi ya kumlea mtoto atakayezaliwa lakini kijana huyo hakufanya hivyo na kuamua kutoroka majukumu ya kumtunza mwanaye.

Kwa upande wake mama wa mtoto Selemani Salumu ambaye anasadikisha kumtelekeza mtoto wake mara kwa mara amethibitisha kumtelekeza mtoto wake huyo na kwenda kwa wanaume na kusema kuwa siku alipoondoka nyumbani kwa mara ya mwisho alielekea  chanzuru ambapo huko alienda kwa Ally Mkubuge akidai kuwa ni rafiki yake . Na kufafanua kuoa  anapotoroka huwa anaogopa kurudi nyumbani mapema kutokana na shangazi zake kumpiga kwa kile anachokitenda cha kutoroka na kumuacha mtoto nyumbani.

No comments:

Post a Comment