Wednesday, July 2, 2014

UJENZI WA KANISA LA AGLIKANA KATIKA KIJIJI CHA DODOMA ISANGA WAKAMILIKA



Diwani wa kata ya masanze wilayani kilosa mkoani morogoro Jonathani Kambikiye ameongoza harambee ya uchangiaji wa vifaa vya ujenzi wa kanisa la Aglikana kijiji cha Dodoma Isanga kilichopo kwenye kata hiyo.
Harabee hiyo imefanyika hivi karibuni baada ya Ibada ya jumapili ambayo imeongozwa na mchungaji Mwegalawa wa kanisa la Aglikana parishi ya zombo na Area Dean wa dinari ya zombo.
Kambikiye ameongoza zoezi hilo  la harambee ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi ambapo waumini wa kanisa hilo la kijiji cha Dodoma Isanga na viongozi na wadau mbalimbali wameweza kukamilisha vifaa vyote kwa ajili ya kuezekwa kanisa hilo ambalo lilianzishwa mwaka 1983 vimeweza kukamilika hivyo kuwa na uhakika wa ujenzi huo wa nyumba ya Mungu.
Vifaa vilivyokuwa vikihitajika ni pamoja na bati 30 mbao 70 na misumari kilo 15 ambapo Diwani huyo amechangia bati tano na kilo nne za misumari ili kuwapa nguvu waumini hao kwa ajili kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo.
Akizungumza  baada ya harambee hiyo Diwani huyo wa kata ya Masanze Jonathani Kambikiye amewashukuru wote waliochangia vifaa hivyo ili kukamilisha ujenzi huo wa kanisa na kuwataka wazee wa kanisa hilo kuhakikisha wanasimamia ipasavyo zoezi hilo la nyumba ya Ibada.

No comments:

Post a Comment