Thursday, July 3, 2014

MBUNGE WA JIMBO LA MIKUMI AWATOA WASIWASI WAKAZI WA MIKUMI JUU YA MRADI WA MAJI MIKUMI WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO


Imeelezwa kuwa licha ya Mwenge wa Uhuru kupita katika Tarafa ya Mikumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo mradi wa maji ambapo mpaka sasa hayajaanza kutoka katika Tarafa hiyo.
                                                        mradi wa maji mikumi

Hayo yameelezwa na baadhi ya wananchi wa Tarafa ya Mikumi Shafii Makiwa na Gaudensia Aloyce wakati wakizungumza na HABARIKWANZA julai mbili mwaka huu.
Wananchi hao wamesema kuwa tatizo la ukosefu wa maji katika Tarafa hiyo ni la muda mrefu kwani tangu Mwenge wa Uhuru kuzindua mradi wa maji safi na salama hadi sasa hakuna jitihada zinazofanyika ili kuhakikisha changamoto ya maji inatatulika katika Tarafa hiyo hali inayosababisha maisha kuzidi kuwa magumu siku hadi siku.
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Mikumi Abdusalama Amer maarufu kwa jina la Sasgas wakati akizungumza na HABARIKWANZA amekiri kutokuwepo kwa maji katika Tarafa hiyo na kuahidi maji yataanza kutoka mapema mwezi wa nane mwaka huu.
                              Mbunge wa jimbo la mikumi Abdulsalama Amer
Amer amesema kuwa sababu ya kutokutoka kwa maji kwenye mradi huo ni kutokana na mkandarasi kuishiwa fedha za kumalizia mradi wa maji kwa wakati lakini kwa sasa fedha imepatikana kwani bajeti hiyo imeshapitishwa Bungeni Mjini Dodoma hivi karibuni.

Aidha Mbunge huyo amewatoa wasiwasi wananchi wa Tarafa ya Mikumi kwa kusema kuwa maji safi na salama lazima yatoke katika maeneo hayo kwani atahakikisha anatatua changamoto zote zinazowakabili hususani ya maji safi na salama. 

No comments:

Post a Comment