Wednesday, July 23, 2014

VIJANA ZAIDI 100 WA CHADENA WILAYANI ULANGA WAJIUNGA NA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM



 BAADHI YA VIJANA AMBAO NI AWALI WALIKUWA WANACHAMA WA CHADEMA WAKIONYESHA KADI ZAO MPYA ZA  CHAMA CHA MAPINDUZI  CCM


Vijana zaidi ya 100 ambao ni wanachama wa chama cha Demokrasia  na maendeleo  CHADEMA    wilaya ya Ulanga  mkoani Morogoro wamekihama chama hicho  na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM).
Pamoja na vijana hao pia Viongozi wa juu wa chama hicho wilayani humo  wakiwemo Mwenyekiti wa wazee wa chadema ambaye  pia ni mjumbe wa halmashauri ya mkoa wa chama hicho ndugu Philipo Zimani na Kaimu mwenyekiti wa chadema jimbo la ulanga mashariki  ambaye pia ni katibu kata wa chadema kata ya ruaha wilayani humo Deodatus Charleswamekihama chama hicho na kujiunga na CCM.
MRATIBU WA WAZEE WA CHADEMA NDUGU ZIMANI  NA  KATIBU KATA WA CHAMA HICHO WILAYANI HUMO DEODATUS CHARLIES, WAKIKABIDHI BENDERA ZA CHAMA HICHO KWA UONGOZI WA CCM.
 
Hatua hiyo ya wanachama hao wa CHADEMA kujiunga na CCM imekuja kufauatia maendeleo mbalimbali yanatekelezwa na mbunge wa jimbo hilo la Ulanga Mashariki Serina Kombani, Kama vile ujenzi wa Barabara na ujenzi wa Soko.
Baadhi ya viongozi wa CCM na wale kutoka chama cha CHADEMA waliokiama chama hicho na kujiunga na CCM
Uwajibikaji wa viongozi wa serikali katika majukumu yao wilayani humo ni moja ya sababu inayowafanya wanachama wa vyama vya  upinzani kurudi chama cha mapinduzi  CCM.

No comments:

Post a Comment