Thursday, July 3, 2014

MKUU WA WILAYA YA KILOSA ELIAS TARIMO AMEWATAKA WAHUDUMU WA AFYA WILAYANI KILOSA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA KAZI WAWAPO KAZINI



Mkuu wa wilaya kilosa mkoani morogoro Elias Tarimo amewataka wahudumu wa sekta ya afya wilayani humo kufanya kazi kwa uadilifu na kufuata maadili ya kazi zao.
Ametoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa kikao na wajumbe wa baraza la wazee wilaya, mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri wilaya,Viongozi wa vyama vya siasa na Baadhi ya wataaramu wa aiadaza za Halmashauri ya wilaya kilosa.
Tarimo ameyasema hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na wazee wa baraza hilo,ya kuwa wahudumu wa afya katika hospitali ya wilaya ,wanatabia ya kuwatolea lugha chafu mara wanapofika kwa ajili ya kupata matibabu hospitalini hapo.
Aidha amesema kuwa wanapaswa kuhudumia wagonjwa kwa kauli nzuri na upendo kwa wagonjwa wanahitaji kupokea na kupatiwa huduma kwa faraja si kuwatolea lugha chafu,ambapo baadhi wamekuwa wakitoa malalamiko kila siku juu ya watoa huduma hao wa sekta ya afya huwafokea na kuwanyanyasa wagonjwa.
Ameongeza kwa kusema kuwa changamoto zinazovikabili vituo vya afya wilayani humo zikiwemo dawa na watoa huduma,amesma serikali itaendelea kuzifanyia kazi changamoto hizo ikiwemo kutoa kipaumbele kwa wazee kwa kuandaliwa kadi za matibabu ili wazitumie mara wanapokwenda kupata matibabu.

No comments:

Post a Comment