Tuesday, July 1, 2014

WAUGUZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA KILOSA WATAKIWA KUWA NA LUGHA NZURI WANAPOWAHUDUMIA WAGONJWA HOSPITALINI HAPO.



 
Chama cha mapinduzi  CCM wilayani Kilosa mkoani Morogoro kimesikitishwa na hali inayojitokeza katika hospital ya wilaya kwa baadhi ya wauguzi wa afya kutoa lugha chafu  kwa wagonjwa mara wanapokwenda kupata matibabu hospitalin hapo.

Hayo yameelezwa na katibu waccm wilaya ya Kilosa Dodo Sambu hivi karibuni wakati wa kikao na mkurugenzi  wa halmashauri ya wilaya baada ya wazee hao kutoa malalamiko kuhusu wagonjwa kunyanyaswa na watoa huduma hao .

 Dodo ameeleza kuwa chama  cha mapinduzi kimepokea  kwa  masikitiko yanayotolowe na wananchi na wazee juu ya vitendo vya kutolewa lugha  chafu  vinavotendwa na watoa huduma hospitalini hapo.

Amesema kuwa  watoa huduma hao wa afya wanapaswa kuhudumia vizuri na  kwa upendo wagonjwa mara wanapofika kupata matibabu kwa kufuata maadili ya kazi zao.
Dodo ameongeza kuwa malamiko ambayo yanayotolewa kwenye kuwahudumia wagonjwa hospitalini hapo yanatendwa  na watoa huduma hao ambao wanasahau  kuwa waliapa kuwahidumia vizuri wagonjwa  hivyo  kufuatia hali hiyo chama cha mapinduzi wilaya kinaiomba halmashauri ya wilaya kuwachukulia hatua  wahudumu hao ikiwemo kupumzishwa kazi.

No comments:

Post a Comment