Wednesday, July 23, 2014

WAZAZI NA WALEZI WANUFAIKA NA SHIRIKA LA HUDESA KATIKA KUPUNGUZA UDUMAVU WA WATOTO NA VIFO VYA KINAMAMA



Shirika lisilokuwa la kiserikali HUDESA linalofadhiliwa na USAID Kwa ushirikiano na AFRICARE linaendesha mafunzo ya lishe bora kwa kina mama wajawazito na wanaonyonyesha kwa lengo la kupunguza vifo vya kinamama wajawazito na watoto walio chini ya umri wa miaka miwili wilayani kilosa mkoani morogoro. 


                           Afisa mradi ustawi wa HUDESA wilayani kilosa Hawa Hatibu

                                   Viazi lishe kwa ajili ya watoto na kinamama wanaonyonyesha

Akizungumzia malengo ya HUDESA julai 22 mwaka huu Afisa ustawi wa shirika hilo wilayani kilosa Hawa Hatibu amefafanua kuwa mwanzo bora ni siku elfu moja akiwa na maana toka motto yupo tumboni hadi kuzaliwa kwake na kufikia umri wa miaka miwili [2]ameeleza kuwa kitaalamu motto anapokosa lishe bora kwa kipindi hicho anaweza kudumaa kiakili na kimwili.
                                                          Bustani ya kiroba

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa katika mpango huo wa mwanzo bora wanafundisha kinamama jinsi ya kuandaa chakula bora kwa mtoto sambamba na hapo wameandaa bustani ya mbogamboga za majani pamoja na viazi lishe ambavyo hutumika kumuandalia chakula mtoto.
                                     Baadhi ya walezi wakiwa kwenye bustani
Kwa upande wake Salehe kaombwe ambaye na mhudumu wa afya wa majumbani kata ya kasiki wilayani kilosa amesema kuwa wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuepukana na vifo vya kinamama na udumavu wa watoto.
                                              Bustani ya mbogamboga aina ya chainizi

Nao baadhi ya kinamama wa wilayani kilosa mkoani morogoro Husna Rashidi na Amina bint Ally wamesema kuwa wanalishukuru sana shirika la HUDESA kwa kuwapatia elimu ya mafunzo ya jinsi ya kuwaandalia lishe iliyobora watoto wao ili waweze kukua vizuri na kuweza kuepukana na magonjwa yanayoepukika.



No comments:

Post a Comment