Wednesday, June 25, 2014

SERIKALI YATAKIWA KUPANGA BEI MAALUMU YA MAZAO ILI KUWAINUA WAKULIMA KIUCHUMI



Wito umetolewa kwa Serikali kupanga bei maalumu kwa wakulima itakayo weza kuleta tija pindi watakapo vuna mazao yao hali itakayo pelekea kuepukana na bei za wafanya biashara ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Wito umetolewa juni 24 mwaka huu na wananchi wa wilayani kilosa wakiongea katika kitao walichokaa na waandishi wa habari kujadili mada iliyokuwa ikisema ni kipaumbele gani kimetolewa kwa wakulima juu ya mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN).
Mmoja wa wananchi hao Skutoka Mgeta ambaye hatukuweza kupata jina lake amesema  kuwa bei wanayouzia mazao yao inapangwa na wafanya biashara   kwani bei zao haziendani  na ghalama za uzalishaji hivo kushindwa kuendesha maisha yao na kubaki kuwa watu wa maisha duni.
Ameongeza kwa kusema kuwa Serikali inatakiwa kuweka mikakati ya bei ya wakulima kama ilivyo kwa wafanya biashara  ili waweze kuepukana na umasikini kupitia kilimo.
Naye mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la Mr Kipala amesema kuwa Serikali iandae soko la kuuza mazao ya wakulima kwa urahisi.na kwamba wasipoweka utaratibu mkulima atazidi kukandamizwa kwani mfanyabiashara atanunua  bidhaa kwa bei anayo itaka kutokana na uwitaji wa mteja.

No comments:

Post a Comment