Wednesday, June 25, 2014

WANANCHI WA KILOSA WAPATA ELIMU KUHUSIANA NA KATIBA



Kituo cha usaidizi wa Kisheria  Paralegal (KIPA) kilichopo Kilosa Mkoani Morogoro kimepokea vitabu vya aina 3 vya usaidizi wa kisheria kutoka Kituo cha Sheria na haki za Binadamu kwa kushirikiana na Twaweza lengo ni kuwaongezea uwezo wa kujitambua wananchi kuhusiana na Katiba mpya na  haki zao.
Akizungumza na HABARIKWANZA ofisini kwake Msaidizi wa Kisheria wa Wilaya ya Kilosa Vimwaya Manyoli amesema kuwa wamepokea jumla ya vitabu elfu ishirini na nne juni 22 mwaka huu ambavyo ni kitabu Katiba ni nini,Twende wapi na Hashuki mtu hapa.
 Amesema kuwa vitabu hivyo ni vizuri kwani vinaelimisha Jamii na wananchi kwa Ujumla pia mtu anaweza kuelewa kwa kuangalia picha zilizomo kitabuni humo na amewashauri wananchi  kuwa na mazoea ya kujisomea vitabu ili waweze kukuza uelewa wao wa Kimawazo.
Aidha ameongeza kuwa wananchi endapo watajenga mazoea na kusema kuwa yaliyomo ndani ya vitabu hivyo yanasadifu maisha yaliyopo sasa. 


No comments:

Post a Comment