Tuesday, June 17, 2014

WANANCHI WILAYANI KILOSA WAHAMASISHWA KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA.



Wananchi wa wilayani kilosa mkoani morogoro wameshauriwa kujiunga na mfuko wa bima ya Afya CHF ili kupunguza gharama za maisha.
Ameyasema hayo mkuu wa wilaya ya kiilosa Elias Tarimo June 16 mwaka huu kwenye maadhimisho ya mtoto wa Afrika ambapo kiwilaya yamefanyika katika kata ya zombo kijiji cha nyali yaliyobeba kauli mbiu isemayo KUPATA ELIMU BORA NA ISIYO NA KIKWAZO NI HAKI YA KILA MTOTO.
Tarimo amesema kuwa kwa kutekeleza kauli mbiu hiyo mtoto anatakiwa kukua katika afya njema na kuwashauri wazazi na walezi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya hiyo itasaidia kupunguza gharama ya kimaisha kwa kuchangia shilingi elfu tano kwa kipindi cha mwaka mzima na serikari itachangia mwanachama  shilingi elfu tano na kufikia shilingi elfu kumi.
Aidha amesema kuwa tatizo la madawa kutopatikana mahospitalini ni kutokana na wananchi wachache kuchangia mfuko huo wa Bima ya Afya CHF na serikali kushidwa kukidhi hitaji la dawa kwa wananchi,Hivyo amewaomba wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kuondokana na tatizo hilo la upungufu wa madawa hospitalini.
Naye meneja wa Mfuko wa Bima ya afya mkoa wa morogoro Bi,Rose Ongara amefafanua kuwa mwananchi anapaswa kuchangia shiliongi elfu tano kwa kaya yenye watu  kumi na kufafanua kuwa kwa hao watu kumi wote watatibiwa kwa hiyo shilingi elfu tano kwa kipindi cha mwaka mzima na kueleza kuwa ni sawa na shilingi mia tano kwa kila mmoja atatibiwa kwa mwaka na kuwataka wananchi kutumia fursa hiyo ili kujiunga na mfuko huo wa bima ya afya.

No comments:

Post a Comment