Tuesday, June 10, 2014

TATIZO LA KUGUSHI NYARAKA NA WIZI WA MITANDAO KUKOMESHWA NCHINI




Mashirika ya umma na binafsi yameshauriwa kuwashirikisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla  katika kufuatilia masuala ya ubadhirifu uliopo katika maeneo yao na kuwajengea mazingira rafiki na vyombo vya dola ili kufichua vitendo vya ufisadi bila hofu .

Mkuu wa Oparesheni maalum za jeshi la polisi SAIMON SIRRO amesema hayo wakati wa kufungua mkutano wa wataalam wanaoshughulikia makosa ya jinai na kugushi kutoka taasisi za fedha ambapo amesema hatua hiyo itasaidia kuokoa rasilimali za nchi na kutoendelea kuporwa na watu wanaojali maslahi yao binafsi.

Kutokana na tatizo la kugushi na wizi kwa njia ya mtandao kuendelea kushamili nchini,  wataalamu wanaoshughulikia makosa ya jinai ya kughushi kutoka katika taasisi za kifedha wamekutanishwa mjini Morogoro kujengewa uwezo juu ya kubaini mbinu mpya za ughushaji ukiwemo ule wa mitandao.

 Shirika la Afrikan union linazishauri wizara , idara  na taasisi zake , pamoja na mashirika ya umma na binafsi kuwalinda wafanyakazi na wananchi wanaofichua taarifa za ufisadi badala ya kuwatishia na kuwaona ni wasaliti.

 Katibu mtendaji wa shirika linalojishughulisha na uchunguzi wa makosa ya kughushi ASFE amesema  lengo la mafunzo hayo ni kuwaongeza ujunzi na weledi watendaji hao.

 Pamoja na kuwepo kwa hatua kali za kisheria kwa wanaopatikana na hatia katika makosa ya wizi wa kugushi lakini bado wizi huo umeendelea kuwepo hali inayofanya nchi kuendelea kuwa maskini huku baadhi ya watu wakiendelea kujinufaisha kupitia njia hiyo ya haraka.

No comments:

Post a Comment